[go: up one dir, main page]

Nenda kwa yaliyomo

Washia

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Pitio kulingana na tarehe 20:34, 17 Agosti 2010 na 88.232.11.156 (majadiliano)
Nchi za Waislamu wengi na madhehebu
Kibichi: Wasunni wengi; Nyekundu: Washia wengi

Washia (pia: Shi'a; kutoka Kiarabu:شيعة) ni dhehebu katika Uislamu. Kufuatana makadirio mbalimbali kati ya asilimia 10 na 20 za Waislamu wote hufuata Shia na wengine walio wengi ni Wasunni. Isipokuwa katika nchi za Uajemi, Azerbaijan, Iraki, Bahrain, Yemen, Omani na Lebanoni Washia ni kundi kubwa.

Neno Shia latokana na Kiarabu shiá't ali (شیعته علی) yaani "chama cha Ali" likimaanisha kundi la wafuasi wa Ali ibn Abu Talib aliyekuwa mkwe wake Mtume Muhammad na familia yake.

Chanzo cha Shia

Washia huamini ya kwamba familia ya Muhammad hustahili kuwa na uongozi kati ya Waislamu. Familia hii huitwa "ahl-al-bayt" (Kiarabu:أهل البيت).

Ali alimwoa mtoto wa pekee wa mtume aliyeishi yaani binti yake Fatima akawa pia baba wa Hassan na Husain wajukuu wa pekee wa mtume . Baada ya kifo cha Ali wafuasi wake walitaka Hasan na Husein kumfuata katika nafasi ya uongozi wa Uislamu wote lakini idadi kubwa ya Waislamu walishikamana na Muawiya

Washia huamini ya kwamba uongozi wa ahl-al-bayt uliendelea kupitia maimamu mbalimbali.

Vikundi

Washia waligawanyika baada ya imamu wa sita Ismail ibn Dschafar kuhusu swali ni nani imamu halali wa saba. Kutokana na farakano hili vikundi mbalimbali vilijitokeza.

  • Ithnashari: ni kundi kubwa kati ya Washia wakiwa hasa Uajemi, Iraki, Azerbaijan na Lebanoni. Huamini ya kwamba imamu wa 12 alichukuliwa na Allah na kwa sasa yuko bila kufa au bila kuonekana.
  • Waismaili waliachana juu ya imamu wa saba. Kati yao wamegawanyika tena
    • Wanizari huamini ya kwamba maimamu wameendelea hadi leo na kiongozi wao ni Aga Khan. Karim Aga Khan IV kwao ni imamu wa 49 tangu mtume Muhammad.
    • Wabohra walioko Uhindi, Pakistan na Yemen huamini ya kwamba imamu wa saba alipotea kwa sababu amechukuliwa na Mungu na yuko bila kuonekana. Imani hii hufanana kiasi na mafundisho ya Ithnashari.

Kutokana na uhamiaji wakati wa karne ya 19 matawi ya Waismaili yamepatikana pia katika Afrika ya Mashariki. Hasa Wakhodja wamejitolea katika mazingira wanapoishi kwa kujenga shule, sahanati na mahospitali vinavyoitwa mara nyingi "Aga Khan".

Kihistoria palikuwa na vikundi vingi vingine kama vile Wafatima waliotawala Misri kati ya 953 na 1171 BK.

  • Wazaidiya ni kundi la Washia walioko Yemen. Waliachana na Washia wengine juu ya imamu wa tano.


Viungo vya Nje